John 19:34-37

34 aBadala yake mmoja wa wale askari akamchoma mkuki ubavuni na mara pakatoka damu na maji. 35 bMtu aliyeona mambo hayo ndiye alitoa ushuhuda, nao ushuhuda wake ni kweli. Anajua kuwa anasema kweli, naye anashuhudia ili pia nanyi mpate kuamini. 36 cKwa maana mambo haya yalitukia ili Maandiko yapate kutimia, yale yasemayo, “Hakuna hata mfupa wake mmoja utakaovunjwa.” 37 dTena Andiko lingine lasema, “Watamtazama yeye waliyemchoma.”

Maziko Ya Isa

(Mathayo 27:57-61; Marko 15:42-47; Luka 23:50-56)

Copyright information for SwhKC